Wednesday, October 29, 2008

Yalofichwa kwa viongozi yalifunuuliwa kwa wasanii.

Lazima kuna atakayebeba laana ya kilio hiki picha toka http://www.edondaki.blogspot.com/
Najaribu kupata pa kuanzia lakini nahisi ntaanza na swali la ni nini hiki?
Alisema Galinoma na nikaandika katika kipengele cha kila Ijumaa cha THEM, I & THEM niki-quote sentensi yake alipoimba "only this time, the downpressor man happens to be my own brother. Africans where are we going from here?". Ndiyo maswali tunayotakiwa kujiuliza kila wakati kwani ni sisi sisi tunaouana kila iitwayo leo kwa kutaka madaraka tunayopangiwa na wasioathirika na vita hivi. Namkumbuka Lucky Dube alipoimba kwenye wimbo wake uliobeba ajina la albamu wa Victims akionesha tofauti ya maovu waliyotendewa Babu zetu na wakoloni na ya sasa ambayo walio nje wanaangalia tunavyochinjana bila huruma akisema"Bob Marley said How long shall they kill our prophets while we stand aside and look. But little did he know that eventually the enemy will stand aside and look while we slash and kill our own brothers, knowing that alreadythey are the victims of the situation. Still licking wounds from brutality, Still licking wounds from humiliation" Kinachosikitisha ni kuwa anayesababisha kilio, majeraha na madhara haya ya kiakili, kimwili na kimazingira ni ndugu yetu. Ambaye anasema anapigania haki ya yule anayemuua. Na kati ya hao ni wale tuwaitao VIONGOZI. Nasio Fontaine aliimba kwenye wimbo wake wa Babylon You Doom alipowazungumzia hawa wanaosimama kupinga vita ilhali silaha zenye nembo za nchi zao ndizo ziuazo watu ambao viongozi wao wanaendelea kuua kwa kisingizio cha kusaka maisha mema kwa wawauao aliposema "babylon you speak of peace yet you make more war, you suppress the innocent to deceive the poor, death and destructions, hungry Baby Mother breasts run dry, yet you plan more war in your private sessions". Akaendelea kusema "you building more bombs and guns, yet babies are dying for hunger. We're the victims of your oppression. Blood of the innocent that you slaughter is upon your hands. You gave the gun, you set the fight, you sit aside and watch the slaughert."
Kuna mengi yaliyosemwa hapo awali na yanaendelea kuimbwa na kusemwa lakini sijui kwanini "viongozi" hawabadiliki na kuthamini utu na utaifa kuliko pesa.
Well. Kuna pande mbili. Ya wenzetu kaka zetu ambazo kwa manufaa yao na biashara za watengeneza silaha wanaamua kutothamini uhai wa wenzao na kuteketeza jamii kwa kisingizio cha kuleta maendeleo nchini mwao. Morgan Heritage waliimba kwenye swimbo wao so much more to come wakisema "these are the days known as eve of destructions, with POLITRIX just leading every nation" na ndilo tuonalo sasa. Wanaoathirika ni wale ambao hata hawajui maana na sababu ya vita. Watoto na kinamama na wenye ulemavu na mahitaji ya ziada ndio wanaobaki kuwa wahanga wa haya machafuko. Kusema hakumaanishi uoga, ila ni kuwa sauti ya wale wasioweza kupata nafasi ya kuandika haya maana wako kwenye mbio za angalau kusogeza dakika za maisha yao.
Kina mengi ya kuandika na kuna mengi ya ku-quote toka kwa wasanii hawa wema walioitetea na wanaoitetea Afrika na pengine wengine wanadhani kuandika haya ni ndoto kwani hayawafikii wahusika, lakini Tanya Stephens alisema "may be hoping for a change is a dream, may be life ain't as bad as it seems, but if dreaming is the best i can do then i'll be dreaming my whole life through." Nami ntaendelea kuota na kuomba kwa kuwa amani ni jambo nimuombealo kila mmoja. Si kwa kuwa naogopa kifo, bali kwa kuwa nawasilisha maneno ya wasanii wanaowasemea wasioweza kufanya hivyo. Lucky katika War and Crime alisema "I' m not saying this, because I' m a coward. But I' m thinking of the lives, that we lose everytime we fight Killing innocent people Women and children yeah Who doesn' t know about the good Who doesn' t know about the wars"

WE NEED TO "RISE UP, WISE UP, WAKE UP AND SHAKE UP"

3 comments:

EDWIN NDAKI (EDO) said...

Napenda sana uchambuzi wako HAI uliojikita katika tasnia ya muziki.

Ipo siku wasiposema hao ..mawe yatasema

EDWIN NDAKI (EDO) said...

Ndugu yangu ukijitahidi kuvaa viatu vya huyo mama ndio utajua jinsi gani anavyoteseka.

Ukizingatia sio sinema ya hollywood ila ni hali halisi inamtokea.

Kilio chake ni kwa ajili ya aliyemgongoni na tumbuni kwake achilia mbali yeye mwenyewe hajui hata anapokimbilia kuna usalama gani.

Hana passport ya kukimbia nchi,wala pesa.

Hana kifaru cha kujilinda.

Hana lolote jema analopata kati ya serikali iliyomtelekeza au waaasi nwanaotafuta roho yake.

Poleni sana wakina mama na watoto duniani koote mnaoteseka kutokana na mamuzi ya watu wachache.

Ipo siku yote yatakwisha.

Tutafika tu

luihamu said...

amani kaka.