Friday, November 7, 2008

Them, I & Them. NASIO .......... Truth Will Reveal

"You see their faces but you never know their thoughts,.. you see their actions but you never know their reactins, Time and Time-alone will prove the story and every eye will see, TRUTH WILL REVEAL"
Nimesema saana juu ya Nasio. Mmoja kati ya "darubini" kali za maisha ya wengi kupitia muziki halisi wa Reggae. Na japo nilimzungumzia wiki iliyopita, basi hapa ninaye tena katika kibao hiki TRUTH WILL REVEAL kutoka albamu yake ya Revolution.
Na namzungumzia kutokana na mambo matatu yaliyotokea wiki hii. Kwanza sitaweza kuweka pembeni historia iliyowekwa na uchaguzi hapa nchini, pili mazungumzo ya amani ya Congo huko Kenya na tatu watuhumiwa wa pesa za EPA waliofikishwa mahakamani huko nyumbani.
Umati mkubwa nyakati za kampeni. Ukitaka kujua wawazalo juu ya mgombea, angalia matokeo. Kama unabisha muulize Mrema (1995)
Kwa hapa Marekani tumeona namna ambavyo uchaguzi umegeuka kuwa funzo kwa wengi. Kuwaonesha kuwa MABADILIKO yajapo hayazuiwi kwa vitisho wala mtazamo wa mtu. Watu walipiga kura za maoni kwa namna ya kuweka uwiano na wengine hata kutopiga kabisa ilhali wakijua walichonacho mioyoni mwao. Hilo liliwapa watu mtazamo kuwa uchaguzi ungekuwa mgumu kiasi na wengine kubashiri mambo kugeuka siku ya mwisho kulingana na "enthusiasm" waliyokuwa wakiiona kwenye kampeni zao. Walilosahau ni hilo lililoimbwa na Nasio ambalo pia nimeliandika hapo juu. Walidanganywa na sura bila kujua mawazo, na kuangalia matendo bila kujua madhara yake na wakati ulipofika kila mtu akafanya kilichokuwa mioyoni na UKWELI UKADHIHIRIKA kiasi hata cha kuwashangaza walioshindwa. NASIO ALIKUWA NA BADO YUKO SAHIHI.
Naona sura sijui wawazalo. Ni amani, ama kumwadhibu mhusika ama posho? Time and time-alone will prove the story. Picha kwa hisani ya Michuzi
Huko Nairobi ambako mazungumzo ya "kutafuta amani" ya Kongo yanaendelea. Na kama ambavyo nimeshasema tangu awali ni kuwa njia m'badala za kusaka amani zinawaweka wananchi wenye uhitaji wa amani hiyo katika wakati mgumu zaidi. Ni mazungumzo ya viongozi kusaka amani yasiyohusisha pande mbili zinazosababisha machafuko. Wamekutana bila kiongozi wa "waasi" kwa vile tu "ni mkutano wa viongozi". Hapa mtazamo wangu ni kama vile "wanasuuza maji" maana kwa kufanya hivyo hutapata maji masafi bali utachafua na yale uliyokuwa nayo. Kukutana na viongozi huku mkimwacha yule mumuitaye muasi akiendelea kuasi na kuua sijui kunaletaje amani kule aliko? Na njia ya kukutana inayotumika ndio iliyokataliwa na serikali kukutana na muasi. Trust me, mkutano ni sehemu yenye amani, usafiri mzuri, ulinzi wa kutosha, mlo mwema na uliokamilika na mavazi mwanana lakini hawa kinamama, walemavu na watoto wanaendelea kudidimia katika maisha ya kutembea kuisaka dakika ijayo wakiwa hai. "Time and time-alone will prove the story and every eye will see". Picha na NYTimes
Wako kwenye "kitimoto' cha EPA. Wanawaza nini? Watasema. Truth will reveal
Sasa hawa watuhumiwa wa EPA nao sijui wanawaza nini vichwani mwao? Ni watuhumiwa na naamini miongoni mwao (kama sio wote) kuna wanaojua ukweli wa tuhuma zinazowakabili. Je ni wao? Kama ni wao walifanya haya peke yao? Ni akili zao ama waliagizwa? Ni kweli kuwa hawa ndio waliochukua mapesa yote? Kuna wengine? Nao ni tabaka la kati kama hawa? Na kama ndio mbona hawaonekani kumiliki na kurejesha pesa zote hizo? Kuna wengine? Ni waheshimiwa? Nasubiri wakianza kuanika ukweli wa mambo. Ni yaleyale aliyoimba Nasio kuwa "you see their faces but you never know their thoughts... time and time-alone will prove the story, and every eye will see. TRUTH WILL REVEAL.

BLESSINGS

**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

1 comment:

Anonymous said...

MSAMA NI TAPELI WADAU HEBU FANYIENI KAZI HILI SWALA KWANI ANAAIBISHA NA KUIBA KUPITIA KIVULI CHA ULOKOLE. KATAPELI JAMAA WA UPANGA MILLIONI SABA.

KATAPELI TBC MILIONI NNE IKIWAPO CHEQUE FEKI NA SASA TBC KUMFIKISHA MAHAKAMANI NA KUMTANGAZA TBC ONE NA REDIONI KAMA TAPELI MLOKOLE FANYENI UTAFITI.