Friday, October 9, 2009

ULEZI........CHANGAMOTO YETU kwa JAMII BORA

Kutokana na CHANGAMOTO zilizo nje ya uwezo wangu, nimeshindwa kuweka kipengele cha Them, I & Them kwa siku ya leo. Ila, nina CHANGAMOTO YETU SOTE KUHUSU ULEZI NA MALEZI
Taswira toka http://co.humboldt.ca.us
Kuna wakati maisha yetu hayaendi kama tupendavyo. Yaani uwezo wa kutimiza ndoto zetu unazidiwa na ukweli wa ugumu wa maisha. Na kwa kuwa hatutimizi malengo yetu, haimaanishi kuwa hatuwezi kuishi maisha mema. Tunaweza kwa KUTAMBUA wapi palipo na uwezekano wa kusaidiwa kutimiza ndoto ama malengo yetu kwan ufasaha na mafanikio zaidi ya tunavyoweza. Ni hapa ambapo tunatakiwa kuwa wasaidizi wa wenzetu. Wa ndugu na jamaa zetu na kuwaonesha njia sahihi ili wafanikiwapo wawe na uwezo wa kutusaidia sisi na jamii kwa ujumla.
Juzi nilikuwa nasoma ukurasa wa rafiki yangu kwenye facebook. Nikakutana na picha njeeema saana ya Mamaye kisha nikaeleza ukweli kuhusu jukumu la kinamama. Aliponijibu nikajikuta nakaribia kutiririsha chozi. Alinieleza kuhusu UPENDO, UJASIRI NA IMANI aliyonayo mama yake. Sikushangaa sana kwani na yeye yuko hivyo. Kisha nikarejea kwa wazazi wengi niwajuao (namtanguliza Mamangu mpenzi) na kugundua kuwa wengi wanafanya mengi ambayo sasa hivi yanaigusa jamii kubwa kuliko ambavyo ingekuwa kama wangeamua kujilimbikizia wao. Najaribu kufikiri kama Mama zetu wangepata muda wa kuelimishana kwa namna tufanyavyo (hata kama wangekuwa na ma-pc kila chumba cha nyumba na muda wa kufanya hivyo). Lakini hii ni sehemu ndoooogo saaaana ya faida ambayo Mama zetu (na wazazi + walezi kwa ujumla) wameiwekeza kwetu na sasa ulimwengu mzima unanufaika.
Niliwahi kuandika kuwa HUWEZI KUWASHUKURU WOTE WALIOKUSAIDIA, BALI WAOMBEE. Waombee kwa moyo wa kuwekeza katika kile unachokitumia sasa kutuelimisha na kutupa changamoto za maisha.
Na hii sasa ni CHANGAMOTO YETU SOTE kubadili mawazo ya u-mimi na kuwekeza katika kile tuwezacho, lakini pia kile tunachoweza kuwawezesha wenzetu na tufanye hivyo.
Narejesha habari hii toka kwake Dr Ben Carson aliyoizungumza katika kipindi cha Morning Edition cha NPR ambapo kila Jumatatu huwa wanaleta watu tofauti kueleza wanachoamini. Yeye alisema anaamini kuwa THERE IS NO JOB MORE IMPORTANT THAN PARENTING. (Bofya hapa kusoma na kusikiliza wengine wasemavyo)
Labda tujiulize kuwa ni matendo mangapi yanayoimong'onya jamii kwa kuwa watu hawakulelewa vema?? Hawakuoneshwa njia sahihi ya kupia, hawakufunzwa kujitambua na kutambua na kuheshimu tofauti na mafanano yetu, hawakuelezwa kuwa sisi ni zaidi ya muonekano, ni zaidi ya pesa, ni zaidi ya mali, ni zaidi ya sifa za mtaani na hata zaidi ya vile ambavyo wasiotujua wanatufanya tujione????
Ni mangapi yanayotokea sasa na kuonekana dhahiri kuwa ni matokeo ya ULEZI M'BOVU???

Naungana na Dr Carson kuwa HAKUNA KAZI ILIYO MUHIMU ZAIDI YA KULEA NA NAWASHUKURU WAZAZI NA WALEZI WANGU WOOOTE WALIONILEA NA WANAOENDELEA KUNILEA (kwa namna moja ama nyingine)
Bonyeza "play" umsikilize na / msome Dr Carson hapa chini

The simplest way to say it is this: I believe in my mother.

My belief began when I was just a kid. I dreamed of becoming a doctor.

My mother was a domestic. Through her work, she observed that successful people spent a lot more time reading than they did watching television. She announced that my brother and I could only watch two to three pre-selected TV programs during the week. With our free time, we had to read two books each from the Detroit Public Library and submit to her written book reports. She would mark them up with check marks and highlights. Years later we realized her marks were a ruse. My mother was illiterate; she had only received a third-grade education.

Although we had no money, between the covers of those books, I could go anywhere, do anything and be anybody.

When I entered high school I was an A-student, but not for long. I wanted the fancy clothes. I wanted to hang out with the guys. I went from being an A-student to a B-student to a C-student, but I didn't care. I was getting the high fives and the low fives and the pats on the back. I was cool.

One night my mother came home from working her multiple jobs and I complained about not having enough Italian knit shirts. She said, "Okay, I'll give you all the money I make this week scrubbing floors and cleaning bathrooms, and you can buy the family food and pay the bills. With everything left over, you can have all the Italian knit shirts you want."

I was very pleased with that arrangement but once I got through allocating money, there was nothing left. I realized my mother was a financial genius to be able to keep a roof over our heads and any kind of food on the table, much less buy clothes.

I also realized that immediate gratification wasn't going to get me anywhere. Success required intellectual preparation.

I went back to my studies and became an A-student again, and eventually I fulfilled my dream and I became a doctor.

Over the years my mother's steadfast faith in God has inspired me, particularly when I had to perform extremely difficult surgical procedures or when I found myself faced with my own medical scare.

A few years ago I discovered I had a very aggressive form of prostate cancer; I was told it might have spread to my spine. My mother was steadfast in her faith in God. She never worried. She said that God was not through with me yet; there was no way that this was going to be a major problem. The abnormality in my spine turned out to be benign; I was able to have surgery and am cured.

My story is really my mother's story -- a woman with little formal education or worldly goods who used her position as a parent to change the lives of many people around the globe. There is no job more important than parenting. This I believe.
N.P.R (National Public Radio)

3 comments:

SHABANI O. KONDO said...

KAKA ULIJUAJE UKWELI MTUPU ULIOTUELEZA.

NDUGU YANGU NIMEREJEA TENA.

Albert Kissima said...

Nashukuru kaka, somo zuri sana.


Niongeze kidogo hapa.
Hatuwezi kurudisha fadhila kwa wazazi/walezi,tuwatumikie wangali bado duniani,kwani itakuwa painful sana pale ambapo utataka kuanza kuwatumikia lakini kwa bahati mbaya wakawa hawapo tena.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Kissima! ni kweli ila kwa wale ambao walezi wao bado wazima wachukue nafasi. Nafasi ndio hii na ni sasa. Asante kwa somo zuri Mzee wa Changamoto kama kawa yako kila wakati ni changamoto tu. Safi sana kuchangamsha watu.