Friday, May 6, 2011

Them, I & Them...AFRICA UNITE....Bob Marley

Alifariki tarehe 11 mwezi wa tano mwaka 1981. Tarehe ya kufariki kwake ni kati ya sababu zinazofanya mwezi huu kusherehekewa kama mwezi wa amani na pia kuwa na matamasha mengi ya kumuenzi Mfalme huyu wa Reggae duniani.
Waweza kuwa na tafsiri yako ya Bob Marley na pengine hata hadhi utakayompa kulingana na mtazamo wako kwakwe, lakini ushahidi wa kazi yake waonesha kuwa alikuwa zaidi ya mwanafalsafa, zaidi ya mtabiri, zaidi ya muona mbali na aliyeona njia sahihi za kuikwamua dunia miongo kadhaa iliyopita, aliyehimiza kuhusu KUJITAMBUA kama njia ya kutuweka huru na askari wa jeshi la amani aliyetumia kazi yake kama silaha halisi.
Aliimba katika wimbo wake aliouita Real Situation kuhusu wanyang'anyi wa mali za watu wanaoamini kuwa "the total destruction is the only solution" na tunaona yatokeayo ulimwenguni sasa. Katika wimbo huo huo alisema "Give them an inch, they take a yard; Give them a yard, they take a mile" akiwaeleza wale ambao wakipata kisa cha kuingia nchini mwako hawatoki na kila siku watakuwa na sababu ya kuendelea kuwepo kuinyonya nchi. Ndio tuonayo leo.
Lakini pamoja na mengi aliyoonya, Bob aliliasa bara la Afrika na wana wa Afrika kuungana kama njia pekee ya kuweza kusonga mbele. Japo wapo waliopinga alilosema (kwa kuhukumu muonekano wake), alilosema lilifanyiwa kazi (kinadharia) takribani miaka 21 baada ya kifo chake. Waligundua ukweli wa alilosema na kujitahidi kujipachika uasili wa wazo japo yajulikana alisema nani, kwanini na ili kiwe nini.
Bob aliweka bayana katika wimbo wake wa AFRICA UNITE kuwa kuna umuhimu na ulazima wa kuungana kikweli kwani twahitaji ku"Unite for the benefit of your children, Unite for it’s later than you think". Kibaya ni kuwa WATAWALA wetu wajiitao viongozi na ambao wana upeo mdogo zaidi ya Bob hawasikilizi usia wa kutupeleka tutakako.Wanacheza POLI=TRIX
Kumzungumzia Bob na nyimbo zake hakuhitaji ukurasa wa pekee, bali blog ama tovuti kamili kwa ajili yake, ila kwa leo naomba tuhitimishe mwezi kwa kumsikiliza katika wimbo huu.

Africa unite:
'Cause we're moving right out of Babylon,
And we're going to our Father's land, yea-ea.

How good and how pleasant it would be before God and man, yea-eah! -
To see the unification of all Africans, yeah! -
As it's been said a'ready, let it be done, yeah!
We are the children of the Rastaman;
We are the children of the Iyaman.

So-o, Africa unite:
'Cause the children (Africa unite) wanna come home.
Africa unite:
'Cause we're moving right out of Babylon, yea,
And we're grooving to our Father's land, yea-ea.

How good and how pleasant it would be before God and man
To see the unification of all Rastaman, yeah.
As it's been said a'ready, let it be done!
I tell you who we are under the sun:
We are the children of the Rastaman;
We are the children of the Iyaman.

So-o: Africa unite,
Afri - Africa unite, yeah!
Unite for the benefit (Africa unite) for the benefit of your people!
Unite for it's later (Africa unite) than you think!
Unite for the benefit (Africa unite) of my children!
Unite for it's later (Africa uniting) than you think!
Africa awaits (Africa unite) its creators!
Africa awaiting (Africa uniting) its Creator!
Africa, you're my (Africa unite) forefather cornerstone!
Unite for the Africans (Africa uniting) abroad!
Unite for the Africans (Africa unite) a yard!
/fadeout/


**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

2 comments:

emu-three said...

Unajua katik hali ya kimaisha unaweza ukawa mtakatifu hata kama haupo katika yale masharti ya kuwa mtakakatifu , kama vile mtu anaweza kuwa mwema hata kama haamini dini...!
\Bob maneno yake yalitosha kabisa kuwa katika kundi la watakatifu au nasema uwongo!, sijui matendo yake, lakini maneno yake katika nyimbo zake mmmmh, mtakatifu!

Unknown said...

@emu-three.

Dini mbalimbali zinaheshimu kwa namna ya pekee watu walio hai au waliokufa ambao walionekana kuwa jirani zaidi na Mungu wakaambukizwa utakatifu wake. Kwa hiyo pengine wanaitwa watakatifu na kutazamwa kama vielelezo vya uadilifu na waombezi.

Katika Uyahudi Jina linalotumika zaidi ni tzadik (mtu wa haki, mwadilifu), aliyejitahidi kufuata Torati.

Kitabu cha TALMUD kinasema kila mara duniani walau 36 tzaddikim wanaishi kati yetu na kuzuia ulimwengu usiangamizwe.

Pengine wanaitwa hivyo hata watu wa mataifa, hasa waliojitahidi kusaidia Wayahudi, k.mf. wakati wa dhuluma.

Mwanzoni mwa Kanisa kila Mkristo aliitwa mtakatifu kwa sababu alitengwa na ulimwengu na kuwekwa wakfu kwa Mungu aliye mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu.

Sifa hiyohiyo ilitolewa pia kwa mahali, siku, vitu n.k. kutokana na matumizi yake ya kidini.

@Mubelwa

Nimekuwa nikipita hapa kijiweni kimya kimya leo nimewiwa kuacha unyayo.

Ahsante kwa kipengele cha Them, I & Them. PAMOJA TUNAWEZA.