Sunday, June 24, 2012

KUAHIRISHWA KWA HARAMBEE YA MSIBA DMV



Kama ambavyo tuliwaarifu hapo awali, Shirika la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kupitia mpango wake wa WESTADI ulithibitisha kugharamia mwili wa Ndugu yetu Domitian Rutakyamirwa pamoja na mwanafamilia mmoja atakayesindikiza mwili, hivyo harambee ya kuchangia gharama za kusafirisha mwili wake iliyokuwa imepangwa kufanyika hii leo haitafanyika tena.

Ibada ya kumuaga itafanyika siku ya Jumatano saa KUMI JIONI katika kanisa la
The Way of the Cross Gospel Ministries.
3621 Campus Drive,
College Park. MD. 20705


Ndg. Domitian aliyekuwa mume wa Dada Bernadetha Kaiza na mkazi wa Washington DC alifariki asubuhi ya Juni 18, 2012 saa mbili na dakika 55 asubuhi (8:55 am) katika hospitali ya George Washington University, Washington DC.

Msiba upo nyumbani kwa familia ya Mr & Mrs Deo Mosha.
Anwani ni:
4402 Hatties Progress Dr, 
Bowie, MD. 20720 

Kwa maelezo zaidi na maelekezo tafadhali wasiliana na:
Idd Sandali (Rais wa Jumuiya ya waTanzania DMV) 301-613-5165 
Henry Kente: 240-938-2452 
Bernadetha Kaiza: 240-704-5891 
Marmetha (Mimi) Kente 301-693-4550 
Mubelwa Bandio: 240-281-0574 

No comments: