Friday, March 8, 2013

Kwani vipaji / fani hufunzwa ama twazaliwa navyo?




Hayati Mzee Jomo Kenyatta na mwanae Hapa ni TASWIRA tu kwa kinaKaka wa familia ya Michuzi. Heshima kwenu. Picha toka Michuzi Blog
Vitali na Vlladimir Klistchko, wao ni mabingwa wa Ndondi wa Dunia Uzito wa juu
Kolo na nduguye Yaya Toure wao ni soka
Laila kama Babake Muhamad Ali
Ralf na nduguye Michael Schumacher wao ni Formula One
Baba na Mwana Bush waliopishana vipindi viwili vya Urais Marekani

Nimekuwa nikijiuliza swali hili kwa muda sasa kutokana na ukweli kuwa sina hakika kama watu wa familia moja hufanya mambo yanayofanana kwa kuwayako ndani ya damu ama kwa kuwa kuna mwongozo mzuri na wa manufaa toka kwa mwanafamilia mwingine ameonesha njia katika hilo?
Unawakumbuka kina Njohole kwenye soka, Uvuruge kwenye muziki na wengineo wengi?
Hebu Tazama hapo kisha unisaidie kujibu.

No comments: