Friday, August 9, 2013

Tamasha kubwa la muziki wa Injili kufanyika Washington DC kesho

Waimbaji wanaofanya vema kwenye muziki wa Injili Afrika Mashariki, Upendo Kilahiro na Christina Shusho, watatumbuiza katika Tamasha kubwa la Injili litakalofanyika Jumamosi hii jijini Washington DC
Kama walivyoongea kwenye VIDEO HII, waimbaji hao wamekamilisha maandalizi ya tamasha hilo ambalo pia litashirikisha waimbaji wenyeji wa hapa Marekani.
Tamasha hilo kubwa lililo sehemu ya Maadhimisho ya miaka mitano ya kanisa la The Way of The Cross Gospel Ministries litafanyika siku ya Jumamosi kuanzia saa kumi kamili mpaka saa tatu usiku (6:00pm - 9:00pm) na kiingilio kwenye tamasha hilo kitakuwa ni dola kumi ($10) kwa watu wazima, bure kwa watoto.
Anwani ambapo litapofanyika tamasha hilo ni
The Way of the Cross Gospel Ministries 
(at University United Methodist Church) 
3621 Campus Drive 
College Park, MD 20740 
Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana na
Mch. Ferdnand Shideko +1 240 476 6718 ama
Ms Flora Mnkande +1 240 217 6335
Waimbaji hawa wote watatumbuiza nyimbo zao za zamani na mpya na wanawaalika watu wote kujumuika nao na waimbaji wenyeji kuweza kupata BARAKA kwa njia hii ya uimbaji

No comments: