Monday, October 14, 2013

Kwako "Babu". Natamani ungekuwepo ukayaona na kuyasikia ya sasa


Shikamoo Babu.
Natumai kwa sala zetu za wewe kuLALA MAHALI PEMA PEPONI utakuwa huko ukipumzika baada ya mengi uliyotenda.
Sasa nimeamka nikasikiliza wengi "wanavyokuenzi", nikaona mimi nisikwambie haya leo, unasikia mengi na pengine mengi yanakufanya ukereke kwa UNAFIKI unaoendelea. Nimeona nikuandikie ili BAADAE SANA ukishapunguza hasira za hawa wakuenzio kwa kuishi usivyopenda zikiisha, usome ujumbe huu.
Babu....
Nangalia uchumi wa dunia unakoelekea na namna mataifa yanavyochukua umiliki wa uendeshaji wa shughuli muhimu za kiuchumi kisha naishia kujiuliza kama hii si sehemu ama aina mpya ya ujamaa?
Ninasoma MAKALA HII ninapata ka-picha kadoogo kwa mbali kuwa kama Mheshimiwa Baba wa Taifa Mwl Nyerere ungekuwepo, basi ungeweza kurejea kusema mawili matatu ambayo ulishawahi kusema miaka kadhaa iliyopita na ambayo yamekuwa katika hotuba zako na nukuhu zilizopo sehemu mbalimbali.
Nawaza......
Ungekuweo leo hii ungesemaje? Hakuna mwenye jibu sahii lakini kwa kuwa ulishaonya kwenye hotuba zako, ninaloweza kuhisi ni kuwa ungekumbusha kile ulichosema ambacho wengi hawakudhani kuwa kingetimia na ungekuwa wakati wa kudhihirika tena kwa maono yako.
Miaka 14 tangu ututoke, bado unakumbukwa na binafsi natamani ungekuwepo ukanona viongozi wengi wa barani Afrika ambao wanayumbishwa misimamo yao na hata kupindisha ilani zao zilizowapa nafasi ya kuwatumikia wananchi, na kuwa kama hawatambui maslahi ya wananchi wao mpaka WAPANGIWE na mataifa makubwa ambayo baadhi ya viongozi wao hawajui lolote kuhusu nchi hizo.
Natamani ungekuwepo ukaona viongozi wetu wa sasa ambao hawawezi kusimamisha mapigano (hata ya RUSHWA) mpaka watishiwe na mataifa fulani, ama wawekewe vikwazo na fulani.
Si unakumbuka ulivyozungumza kuhusu RUSHWA?
Wengine hawakukusikia, wengine walipuuza, wengine wanafanya kile ambacho sisi huku tunaita "kupotezea"
Ngoja niwakumbushe hiki kisha tuendelee.

Natamani ungekuwepo ukaona viongozi wasiothamini uhai wa wananchi wao kwa kuendeleza vita baina ya wanachi wa nchini mwao mpaka waamriwe kuacha na mataifa ya nje.
Yaani wa kuhimiza kuhusu UCHAPAJI KAZI wamemomonyoka saana. Siku hizi ni MWENDO WA AHADI utadhani wana pesa ya kuibadili nchi.
Hawategemei RASILIMALI WATU. Na wanasahau hata mfano uliowahi kuwapa kipindi kile wa JFK
Najua watanichukia kusikia nawakumbusha, ila........nawakumbusha

Ungekuwepo basi ungeona viongozi wanaotumia mwanya wa elimu na mfumo m'bovu wa utawala kujilimbikizia mali kwa jasho la wahitaji (sio maskini) wengi Barani mwetu.
By the way, hayo ni ya Afrika kwa ujumla, ya nyumbani Tanzania yanasikitisha zaidi. Utayasoma kwingine ukipata nafasi.
Ngoja....
Babu, ni kama vile kila mtu nasaka kufika pale ambapo wewe ulisema ni MZIGO.
Lakini siku hizi wanavyopakimbilia. Naamini uchaguzi wa 2015, tutakuwa na karatasi ya kura yenye maneni P.T.O.
Sijui wanapajua kweli ama wanadhani kwa kuwa watakuwa WATAWALA WAKUU basi watafanya watakalo?
Wakumbushe Babu..Wakumbushe

Kibaya zaidi, ka-mchakato ka kuelekea huko kwenye urais kameanza kunuka uDINI na hata uKABILA.
Yaani...natamani ungekuwepo ukawaambia. Japo nina mashaka kama wangesikiliza. Kwani si ulishawaambia?
Najua kuna wanaobisha, ngoja niwawekee ulilosema

Ni viongozi wachache tunaoweza kujivunia na ambao msimamo wao unaendelea kuonekana kuwa wazi na usioyumbishwa na "viranja" wa dunia. Wengi wanamjua Mandela kama kiongozi hodari, shupavu na jasiri katika Afrika na wengi wanakubaliana na hilo, lakini pia kama alivyosema Mchambuzi na Mwandishi hodari Freddy Macha, kabla ya Mandela alikuwepo Nyerere na ujasiri, uwezo na upeo wako bado unaheshimika miongoni mwa wengi.
Tunakanganywa na hawa uliowaacha ambao HATA SIKU MOJA HAWAJAKIRI WALA KUWAJIBIKA KWA MAKOSA YAO.
Wakikosa wa kumsingizia nchini, watamsinginzia aliye nje. Na sikwambii kitu kipya....si unakumbuka ulipozungumzia kuhusu KODI?
Wewe unakumbuka Babu, wacha niwakumbushe hawa wanaochagua la kusahau (hasa linapowahusu)

KAMA UNAYAONA HAYA NA MENGINE MENGI BASI ENDELEA KUTUOMBEA NA KAMA HUYAONI BASI TWAKWAMBIA YALIYOPO LAKINI KAMA HUTUSIKII, NDIO MAANA TUNAENDELEA KUTAMANI TU KAMA UNGEKUWEPO.
Anyway Babu......
Ulitekeleza sehemu yako na huko uliko PUMZIKA KWA AMANI.

No comments: