Monday, October 14, 2013

UJINGA ndani ya busara za UWEPO wa Mwenge

Hiviiiiiiiii.....................
Mmeona picha za MAPOKEZI RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA ALIYEKWENDA KUZIMA MWENGE kule IRINGA?
Hapa ndipo palipo na UTAMU wa SIASA. Ambao hauna tofauti na TEKNOLOJIA
"MFANANO" wavyo watokana na ukweli kuwa vinatufanya tujihisi tuko karibu ilhali vinatutenganisha zaidi.
Sasa......
Siasa zinasema ziko pale KUTUJENGA
KUENDELEZA UMOJA WETU...
Na katika tukio MUHIMU AMBALO NDIO ISHARA PEKEE YA UMOJA WETU....WATU WANAVAA SARE ZA KUWATENGANISHA KIITIKADI.
NI AIBU
 
 Kwa Tanzania...
MWENGE NDIO KITU PEKEE CHA KITAIFA KINACHOZUNGUKA KOTE KILA MWAKA.
Na natamani kama MWENGE ungekuwa ukitumika kama SANDUKU LA MAONI ambalo (kwa kuzunguka nchi nzima) tungehakikishiwa maoni ya nchi nzima.
Sina tatizo na NIA YA MWENGE, japo NINA TATIZO NA UTEKELEZAJI WA NIA HIYO.
Hii ilitakiwa iwe siku ambayo TUNGEONA NA KUJIVUNIA UMOJA.
Lakini ona mambo tunayojivunia...
NI AIBU KWETU KAMA TAIFA.
Siamini kama hii ni ishara ya kukua kwa demokrasia...ni ishara ya kumomonyoka kwa UMOJA ambako (kwa bahati mbaya) wapo wanaoonekana kufurahia
SHAME ON US!!!!!!! 
I mean, SHAME ON WAO wanaoendekeza mgawanyo wa hivi....
Well...na wale wote wanaojivunia mgawanyiko huo)
Picha kwa hisani ya kurasa za facebook za Maggid Mjengwa na Liberatus Mwang'ombe


Tanzania Yangu ni kipengele kinachozungumzia ytale yaendeleayo nchini Tanzania na namna ambavyo "ndivyo sivyo" inavyozidi kupamba moto nchini. Kwa matoleo yaliyotangulia BOFYA HAPA
Tuonane "Next Ijayo"

No comments: