Wednesday, October 28, 2009

Wapi ulipo "mstari mwembamba" kati ya UBISHI na IMANI?

Pichani ni rafiki yangu DiJaro ambaye kwa sasa ni kati ya wale wafanyao vema pale TBC Fm. Na miaka ya mwanzo ya 2000 nilibahatika kufanya kazi naye pale Times Fm. Kwa bahati mbaya, wapo waliokuwa wakimkatisha tamaa saaana na kujaribu kumzuia kutekeleza "ndoto" zake. Lakini mara zote tulipokuwa tumeketi nje ya studio (ambako kulikuwa na benchi) tuliongea mengi na kupeana moyo na mara zote alionekana KUAMINI KATIKA AAMINICHO na alikuwa akiamini kuwa yeye ni bora kuliko walivyokuwa wakimuona na tatizo kubwa ni kuwa hakuwa amepewa nafasi ya kuonesha uwezo wake halisi.

Katika vipindi vya Matukio ya wiki na Michezo nilivyobahatika kuongoza pale Times Fm, DiJaro aliweza kushiriki mara kadhaa na kwa hakika alionesha alichokuwa akiamini. Lakini si kwa waliokuwa wakiamini vingine kwani kwao, DiJaro hakuwa na uwezo.

Baadae "alipotea" ambako sikujua nami "nikapotelea" huku nilipo ambako sina hakika kama anajua niliko. Lakini nikasikia namna ambavyo aliendelea "kukua" na kuwa alipata nafasi ya kazi PRT na nikaanza kumsaka na naendelea kumsaka. Hiyo ilikuwa zaidi ya faraja kwangu kwani aliweza KUDHIHIRISHA alichokuwa akijariu kuonesha kwa muda mrefu bila mafanikio.

Mimi na yeye TULIAMINI KUWA ANA UWEZO MKUBWA KULIKO ALIVYOKUWA AKIONEKANA AMA KUDHANIWA na kwa wale waliompinga na kumkatisha tamaa walidhani hakuwa na uwezo bali ALIBISHA UKWELI KUWA HANA UWEZO.
Ni wapi ulipo mstari mwembamba utenganishao UBISHI kama alioonekana nao DiJaro (ambao kwa hakika hana) na IMANI aliyokuwa nayo kuwa yeye ni bora kuliko wanavyomdhania?

Na habari ya rafiki yangu huyu yaniacha nikijiuliza kuwa ni wangapi wanaoishia njiani wakikatishwa tamaa na wasiojua uwezo wao halisi? Ni wapi ambapo tunaweza kuona ulipo mstari mwembamba wa wale wasiokutakia mema na wale wakuoneshao njia sahihi?
Nawaza tu
Hongera Kaka DiJaro na huko uliko, KAZA BUTI
Blessings

4 comments:

Simon Kitururu said...

Inawezekana hakuna mstari! Kuna wakati unajifunza kitu kingine wakati unabisha kwa kutumia hoja nyingine!

chib said...

Cha muhimu, wanasema iwapo unajiamini katika jambo, kamwe usikate tamaa.

viva afrika said...

kusimama imara katika kile uaminicho ndio njia sahihi ya kulinda na kuboresha ulichonacho.

Fadhy Mtanga said...

If u have the motivation,
nothing can stop u, from achieving what u want.

Bravo kaka!