Sunday, February 27, 2011

Kuwezesha chanzo cha tatizo ili kupata suluhisho?..Kwanini????

DAWA YA MOTO NI MOTO.... PHOTO CREDITS: CNN.com
Si ndio WAHENGA (wanaopingwa na Kaka Kamala) walivyosema? Basi kuna ambao wako tofauti kidoogo na Kakangu Luta Kamala ambao wanaamini kuwa unaweza kuzuia vurugu kwa kuwekeza katika chanzo cha vurugu. Mmmmhhhhh!!!!!!!!!!!
Yeah... Majimbo mawili hapa nchini Marekani yako kwenye mjadala mnono wa kuwawezesha wanafunzi na waalimu wa vyuo vikuu KUJILINDA KWA KUINGIA MADARASANI WAKIWA NA BASTOLA.
MJADALA HUU WA TEXAS na HUU WA ARIZONA yaonekana kuzidi kuchukua taswira mpya kila uchao kutokana na BIASHARA ya silaha kuwa kubwa hapa nchini, suala zima la HAKI YA MSINGI YA RAIA KUJILINDA na pia kutokana na matukio kadhaa ambayo yamekuwa yakijitokeza kwenye shule na vyuo kadhaa hapa nchini.
Lakini nawaza kuwa hawa wanaoamini kuwa kila mwanafunzi na mwalimu akiwa na silaha ndio kutakuwa na usalama WANAWAZA NINI?
Nawaza kama watu wenye matatizo ya kushindwa kuzuia hasira zao watakuwa ni sehemu ya usalama ama hatari vyuoni?
Vipi wale wanaochukia watu na kufanya maamuzi ya papo kwa hapo?
Na ile sheria ya "kuua kwa kutokusudia" kwa kuwa umeua ndani ya muda mfupi wa kukerwa itakuwaje hapa?
Maana ukimuudhi mtu hahitaji kwenda mbali kutafuta silaha (ambapo mwendo huo waweza kumfanya awaze mara kadhaa juu ya kile anachotaka kufanya), bali ni kuingiza mkono mfukoni na kufyatua.
Mmmmmmmhhhh!!!
Vipi kuhusu suala zima la shabaha? Vyuo vina maelfu ya wanachuo, na kama kila mmoja atajaribu kumlenga mmoja anayetaka kuua watu, na shabaha isiwe sawia, nahisi "waokozi watauana na kuua watu wengi kuliko ambavyo mmoja anayezuiwa angeua"
WALIOFIKIRIA HILI KUWA SULUHISHO WALIWAZA NINI?
Achana na hao....
Jana nilitumiwa ujumbe huu wa barua pepe na rafiki yangu aliyeweka maswali kadhaa ya KWANINI?
Na alinifanya NIWAZE ZAIDI YA KUCHEKA na kuwaza ALIYEANDIKA HAYA ALIFIKIRIA NINI?
Labda kuna ukweli (yawezekana usiuone kulingana na mazingira) lakini FIKIRIA FIKRA ZA MWANDISHI....ALIWAZA / WALIWAZA NINI?
PHOTO CREDITS: Kinesis Marketing UK
.Why do supermarkets make the sick walk all the way to the back of the store to get their prescriptions while healthy people can buy cigarettes at the front?
.Why do people order double cheeseburgers, large fries, and a diet coke.
.Why do banks leave vault doors open and then chain the pens to the counters.
.Why do we leave cars worth thousands of dollars in our driveways and put our useless junk in the garage.
EVER WONDER ...
.Why the sun lightens our hair, but darkens our skin?
.Why can't women put on mascara with their mouth closed?
.Why don't you ever see the headline 'Psychic Wins Lottery'?
.Why is 'abbreviated' such a long word?
.Why is it that doctors call what they do 'practice'?
.Why is lemon juice made with artificial flavoring, and dish washing liquid made with real lemons?
.Why is the man who invests all your money called a broker?
.Why is the time of day with the slowest traffic called rush hour?
.Why isn't there mouse-flavored cat food?
.Why didn't Noah swat those two mosquitoes?
.Why do they sterilize the needle for lethal injections?
.You know that indestructible black box that is used on airplanes? Why don't they make the whole plane out of that stuff?!
.Why don't sheep shrink when it rains?
.Why are they called apartments when they are all stuck together?
.If flying is so safe, why do they call the airport the terminal?

***"Waliwaza nini ni kipengele cha kuelimishana tukifurahia. Hiki kitakuwa kikikuletea habari za kweli na kushangaza kuhusu watu ambao wamefanya yale ambayo unaweza kujiuliza kuwa WALIWAZA NINI? wakati wanatenda haya.
Kitakuwa na habari fupifupi kutoka ulimwenguni kote. Kwa habari zaidi kuhusu kipengele hiki
BOFYA HAPA"***

Friday, February 25, 2011

Them, I & Them....CRY NO MORE....Beres Hammond

Hali ya maisha ilivyo sasa ULIMWENGUNI imemuathiri takribani kila mmoja. Wengi wamepoteza kazi, wengi wamepoteza ndugu ambao kwa msongo wa mawazo na kukata tamaa wameamua kukatisha maisha yao (na wengine ya wenzi na familia zao) na wengine kuteteresha afya zao kwa kuwaza kuliko wanavyoweza kuwa suluhisho.
Nami kama wengine niliwaza na kuwazua lakini nikagundua kuwa kuna baadhi ya mambo ambayo kuwaza na kufikiri hakutayabadili, bali cha kufanya ni kubadili mfumo wa maisha ulio tegemezi kwayo na kuishi bila kutegemea saaana uwepo wa hayo. Mfumo huu mpya wa maisha una msaada sana kwa sasa hasa kwa yeyote ambaye hana lolote analoweza kufanya kubadili uhalisia wa maisha ya sasa. Baadhi ya mambo hata ukiwaza na kujikwaza hayatabadilika kwa sasa, mfano kuwaza kazi / ajira wakati hakuna anayeajiri, kuwaza nyongeza ya mshahara wakati waajiri wanapunguza watu kazi, kuwaza kuongeza wateja katika biashara wakati wanunuzi wanaishi kwa kuomba na kwa msaada wa serikali, kuwaza pesa mara mbili ya mshahara ilhali unajua halitakoea. Jawabu nililopata naamini ni muafaka kuwa TWAHITAJI KUISHI KAMA TULIVYO NA KUJITAHIDI KUTENGENEZA NAFASI NJEMA YA MAISHA TULIYOPO KULIKO KUENDELEA KUOTA YASIYOWEZEKANA KUTENDEKA SASA. Kwa kifupi twatakiwa kuishi kwa namna tulivyo na si tutakavyo. Kama alivyosema "mwana mpotevu" kuwa Pa kuanzia ni pale ulipo (Bofya hapa kumsoma)
Niungane naye Beres Hammond katika kibao hiki NO MORE ambapo naye ameeleza alivyoamua kuishi bila hesabu za kile asichonacho.
Sote twaweza na itatupunguzia hali ya kujiona kama walioshindwa kuyakabili maisha kwani tutakuwa tukiishi kwa uhalisia wa maisha ya sasa.
Msikilize hapa Beres Hammond anapoanza kwa kusema
"Am gonna cry no more, i've shed my last tear,
No more worrying about what tommorow bring.I'm gonna live today the best way the best way i will have, and from now on that's how is gonna be...."
pia anaendelea kuimba kuwa
" i'm wont set myself for the worry about what i can't have
i'll have to live without......"


**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

Thursday, February 24, 2011

Ubora wa jela ni nini na zetu ni namba ngapi?

Najua tuna viwango vya shule na kwa kutumia vigezo kadhaa tunaweza kupewa orodha ya shule kwa ubora. Naweza kuhisi kuwa wanaangalia uwiano wa idadi ya wanaofaulu, wanaochaguliwa kuendelea na masomo, wanavyopata ujuzi kwa wale wasomeao fani mbalimbali na hata mazingira na maisha baada ya chuo ama shule. Najua hata vyuo kama vya habari ama sheria ama uinjinia huwa vinaheshimika kwa kuangalia ni nyota wangapi wanaofanya kazi zao vyema ambao wamepitia katika vyuo ama taasisi hizo.
Sina hakika na Magereza. Ila nijualo ni kuwa sijawahi soma ushuhuda wa mfungwa yeyote ambaye amefanikiwa kutoka jela na kusema maisha ya kule yalikuwa ya kumuendeleza na kumfanya kuwa raia mwema akitoka na kurejea uraiani. Si mnakumbuka mahojiano ya Mhariri wa zamani wa gazeti la Family Mirror Bwn Zephania Musendo aliyofanya hivi karibuni mara baada ya kutoka jela alivyosimulia mateso kuliko mwongozo wa maisha mema ukitoka jela? Alivyoeleza katika mahojiano yake na Mzee wa Sumo Mpoki Bukuku, unaweza kupata picha ya maisha yalivyo na imani ama mtazamo kwamba kinachobadilisha maisha ya mfungwa jela za nyumbani ni MATESO na si mbinu mpya za kujiajiri mara utokako jela. Sehemu ya mahojiano hayo ni hii hapa akisimulia siku mbayo imemuumiza na kumfedhehesha alipokuwa jela, alisema kuna siku upekuzi wa kawaida katika gereza ulikuwa ukifanyika na wafungwa wote walitakiwa kuvua nguo zote na kuchuchumaa.
“Tulitakiwa kuruka kichura, nilipojaribu kuruka na hii hali yangu (ya ugonjwa) nilidondoka chini. Nilitarajia kuwa mtu wa kwanza kunisaidia angekuwa daktari wa jela, ambaye alikuwepo sehemu hiyo. Lakini hakufanya lolote na niliachwa nikigalagala chini.”“Roho iliniuma sana kwa kuwa Bwana Jela pia hakujali bali alisema hakuna taabu na kuwa mimi nilikuwa nazuga tu”.Anasema, alifikiria pale alipokuwa amelala akiwa uchi, kila mtu alikuwa akimwangalia, na kwa kuwa gereza hilo halikuwa na ukuta, basi hata watu wakiwamo wanafamilia wa askari waliweza kumwona.
“Sitasahau siku hiyo kamwe.”
Ni mateso ambayo tumeyasikia na kuyaona kwa mahabusu (kama Wajelajela) wafungwa, na hata watuhumiwa ambao hawajathibitishwa kuwa na hatia ambao wanapigwa na kuteswa badala ya kupewa njia mbadala za kuendesha maisha yao wakitoka jela. Labda sera za jela ni tofauti kulingana na nchi lakini ningetaraji ziwe kama "vyuo vya mafunzo" kama nisikiavyo wakiita ndugu zetu wa Visiwani lakini si mafunzo ya askari kuangalia uwezo wao wa kutesa, bali kuwaonesha waliowekwa huko kuwa huo ni wakati wa kutafakari huku wakipewa "options" za kujifunza yale yanayoweza kuwasaidia watakapokuwa huru na hasa shughuli za kujiajiri maana unajua ajira inaweza kuwa ngumu kupata ukitoka jela.
Ninaangalia baadhi ya nchi zinavyobadili ama kuwawezesha wafungwa wake kubadilika na baada ya hap[o wanakuwa nyota si tu katika familia zao, bali jamii iwazungukayo, nchi na ulimwengu kwa ujumla. Na kwa kuwa mimi ni mpenzi, mfuatiliaji na mshiriki wa ndondi, wacha niwape mifano ya wafungwa waliobadilika na kuwa nyota katika mchezo huo ulimwenguni. Unawakumbuka ama kuwafamu kina Dwight Muhammad Qawi, Ron Lyle, Mike Tyson na hata Bernard Hopkins? Nimzungumzie Bernard Photo Credit: Bernard Hopkins.net
ambaye bado anapigana na hivi karibuni alimpa kipigo cha kwanza mkali Kelly Pavlik. Amenukuliwa akisema kuwa jela haikumbadilisha bali alibadilika mwenyewe lakini hatuwezi kupinga ukweli kuwa katika miaka aliyokaa jela alishiriki mapambano na michuano kadhaa ya ridhaa iliyomfanya awe bingwa mara tatu akiwa huko na kumpa uzoefu na upenzi zaidi wa mchezo huo ambapo alipotoka aliendelea nao na kuwa yota kwa kushikilia ubingwa kwa zaidi ya miaka 10 mfululizo. NiFuture Hall of Famer na sio tu kaleta heshima kwake, bali kwa jamii ya Philladelphia na pia kwa taifa zima. Anapendwa na vijana wengi na wengine wameanza "carrer" yao ya boxing kwa kupenda upiganaji wake na kwa kuwa wamepata nafasi katika gyms atumiazo.

Bwn HARUNA Pembe Mgombela
Labda sipati taarifa hivyo niwaulize walio walio nyumbani, kuna habari za wafungwa kugeuka kuwa mashujaa wa Taifa? Zaidi ya Bwn HARUNA Pembe Mgombela (54) ambaye alihitimu digrii yake gerezani?
Labda tumsake TID aliyeamua kujiita Sauti ya jela atueleze "kwa sauti" juu ya kilichopo huko.
Nisikimbie swali, UBORA WA JELA NI NINI NA ZETU NI NAMBA NGAPI?

Ni mtazamo tuuuuuu.......See you "next ijayo"

Wednesday, February 23, 2011

Kizazi...Nini kipimo chake? Wakati, Mazingira ama Nyenzo?

Photo Credits: Jack Graham Blog
Labda wapo wanaoshangaa kuwa mtu na mzazi wake wanahesabika kuwa watu wa vizazi tofauti licha ya kwamba wote wako hai.
Wengine wanakubali kuwa wao na wazazi na wazazi wa wazazi wao ni vizazi tofauti licha ya kwamba wote wako hai.
Lakini wapo ambao pengine bila kufikiria wanaamini kuwa kila UZAO ni KIZAZI.
Na pia wapo ambao wanaamini kuwa yachukua miaka mingi kutoweka kwa kizazi kimoja kwenda kingine.
Kwani kila siku si tunasikia muziki huu wa "bongo flava" ukiitwa muziki wa kizazi kipya? Hata kama anayeuimba amevutiwa na muziki miaka michache iliyopita baada ya kumsikiliza "mkongwe" ambaye (kwa tafsiri "yao") si mtu wa kizazi chao?
Hujasikia wasanii wakirudia nyimbo za miaka kadhaa iliyopita na kusema wamezirudia katika MUZIKI WA KIZAZI kipya katika harakati za kutenga kizazi cha "remix" na MUZIKI HALISI?
ACHANA NA HAYA....
Juzi tukiwa shuleni katika kujadili KIJANA NA TEKNOLOJIA, binti mmoja akasimama na kuchangia akisema "maisha yangu yote sasa ni elektroniki. Ndio kalenda, kumbukumbu, miadi, barua, simu, sauti nk. Vyote nafanya kwenye simu yangu ya Iphone." Hapo mie nikawa natikisa kichwa kukubaliana naye. Kisha akasema KWA KIZAZI CHA SASA HUWEZI KUISHI BILA NYENZO KAMA IPHONE.
Hapoooooooooooooooo sasa....Sikusubiri "kunyoosha mkono"
Nikamuuliza kuwa anaamini kuwa kila pembe na mtu / kijana wa rika yake anaijua Iphone achilia mbali simu hata ya kukoroga?
Nikamuuliza anaposema KIZAZI CHA SASA anamaanisha katika nyumba, kijiji, mkoa ama jimbo analoishi ama anamaanisha ULIMWENGU MZIMA?Ni kweli kuwa binti huyu wa miaka 18 wa hapa Maryland yupo kwenye kizazi tofauti na binti ya jirani yetu mwenye miaka 18 pale Bushasha? Kama wana umri sawa, si wako kizazi kimoja? Lakini kama hawatumii nyenzo moja kutokana na mazingira, ina maana mazingira ni kigezo? Na je, ni kweli kuwa "Uncle" nanilii anayetumia kompyuta saana pale Bongo atakuwa katika kizazi sawa na haka kabinti ka hapa kwa kuwa nyenzo zainawaweka kwenye "usawa" wa matumizi?
Ndipo nilipopata wazo la kuja kuuliza hapa kwamba KIZAZI....KIPIMO CHAKE NI NINI? NI WAKATI, MAZINGIRA, AMA NYENZO?Labda nikuonyeshe tu kuwa.....................Hawa hapa chini
Photo Credits: Broadcasting Corporation of China
Ni wanafunzi wa elimu ya awali kama ilivyo kwa hawa hapa chini.
JE!! Japo wanaweza kuwa na umri unaolingana ama kukaribiana, unaamini wako katika KIZAZI KIMOJA?Kwani kizazi ni nini?
Innocent Galinoma aliuliza "what is life? Is life a gift, or a test, or a punishment for my people?"
MSIKILIZE

JUST THINKING OUT LOUD.

Monday, February 21, 2011

Namba moja na Mbili zangu...Si "REMIX"

Ndioooo...Enzi zetu za UZEE WA UJANA....Yaani ni "Enzi zijazo". Upo hapo????
Sina hakika kama ni sahihi kwa wimbo unaorudiwa "UPYA"na msanii kuitwa REMIX, lakini ninafurahi kuona baadhi ya wasanii wana uwezo wa kutunga huku wakiona mbali kwa kuweka MUENDELEZO wa nyimbo zao.
Ni jumatatu, ambapo mara nyingi huwa tunapata nyimbo za kale kuhusiana na maisha ya sasa. Lakini kwa siku ya leo, naomba nikushirikishe nyimbo kadhaa (ambazo zaweza kutokuwa za kale sana) lakini zenye muendelezo mwema wa "hadithi" inayoimbwa.
Na hizi si nyimbo pekee zenye muendelezo, lakini ndizo nilizoona vema kushiriki nanyi.
Tunanze na Vijana Jazz Band.
Katika wimbo wao PENZI HALIGAWANYIKI (sehemu ya kwanza) wanazungumzia RUHUSA aliyopata Mume kuoa mke wa pili, lakini anaonekana kuvunja ahadi hiyo na kuhamishia penzi lote kwa mke wa pili. SIKILIZA

Katika sehemu ya pili, wanaimba juu ya muonekano mpya alionao mke aliyeachwa kiasi cha kutamaniwa na mume wa zamani.
SIKILIZA

Kisha tuhamie kwa ROGATI HEGGA almaarufu kama KATAPILA

katika wimbo FADHILA KWA WAZAZI aliimba sehemu ya kwanza akizungumzia NIA YA KUWALEA WAZAZI.
MSIKILIZE

Lakini kwa bahati mbaya, wazazi hao wakafariki kabla hajatimiza nia hiyo. MSIKILIZE

Na mwisho tumsikilize MUUMINI MWINJUMA
ambaye akiwa na African Revolution na Double M Sound alitoa wimbo wa Mgumba sehemu ya kwanza na ya pili.
Sehemu ya kwanza ilikuwa ni kuhusu kukosa mwana kwa mwanamama huyu, MSIKILIZE

Na sehemu ya pili ilikuwa ni matokeo ya "nani alikuwa mgumba kati ya mume na mke"
MSIKILIZE

** Zilipendwa ni kipengele kinachokujia kila Jumatatu kukuletea muziki wa kale kuhusisha na maisha, muziki ama sanaa ya sasa katika nyanja mbalimbali. Unaweza kusikiliza nyimbo nyingine ndani ya kipengele hiki kwa kubofya hapa, ama mtandao shirika hapa**

Sunday, February 20, 2011

Jelani Film Premiere. Sunday March 13, 2011 at 7:00pm [ET]. BETHESDA, MD


Exclusive Film Premiere
Jelani
Written by Omar Chase Kaseko & Sasha Ryan
Directed by Omar Chase Kaseko
Produced by Kali Imagez & Ashes Film Production

Jelani tells the story of an inter-cultural relationship between
an African immigrant from Tanzania and an African-American woman
living in the United States. The film illustrates significant differences and tensions between
these two communities, addressing complex factors to include gender, class, and education.

The movies at Montgomery mall
7101 Democracy Blvd
Bethesda, MD

The link to buy tickets online :
http://jelanipremiere.eventbrite.com/

Saturday, February 19, 2011

MAKE A CHANGE......Bushman

"If we don't change our values and re-arrange our systems, we'll always gonna be another victims......"

"contradicting themselves in their every illustration, and make me believe in their world of confusions" "treating our people like they're gabage, and through lost of vanity we never seem to aknowledge......now it's time for us to re-enforce ourselves. Who's gonna do it for US? NONE BUT OURSELVES"
Hawa juu ni kina sisi wakiondoka "eneo la tukio"

Na huyu juu ni "yeye" alipotoka "eneo la tukio"

Kutambua watoto waliopotea / kupotezana na wazazi wao

Labda hakuna wa kulaumu kwa kuwa wa kulaumiwa ndiye mlaumu.
Labda HAKUNA ATAKAYEWAJIBIKA kwa kuwa NI DESTURI YAO.
Na sasa tumsikilize BUSHMAN katika wimbo MAKE A CHANGE

Photo Credits: Michuzi Blog, Full Shangwe Blog, Global Publishers Web.

Tuesday, February 15, 2011

Nguvu ndani mwetu...Yenye u-siri wa mafanikio yetu na wenzetu

Nimekuwa nikijaribu kuzifuatilia NGUVU ZILIZO NDANI MWETU ambazo zaweza kuwa CHANYA maishani mwetu na kwa nyakati tofauti nimeandika juu ya kile nilichotambua ama kutambulishwa ambacho ingetufaa sote. Na leo narejea kwenye mazungumzo ya kile ambacho tumeshakisoma kwenye mabaraza yetu mara kadhaa lakini nimekisikia tena kwa NGUVU ZAIDI. Nikukumbushe kilichowahi kusemwa
"Kwa washauri au counselors, watu kibao hulalamika juu ya ukosefu wa amani, upendo na utulivu. Swali la kwanza unaloweza kuwauliza hao walalamikiao wengine kuwa wanawanyima amani ni je, wewe uko katika amani na wewe mwenyewe? Au una amani binafsi?

Swali hili lina maana kuwa amani ya kweli imo ndani mwako na hakuna awezaye kukupa wala kukunyanganya amani hiyo japo wengi hatuna na tunaitafuta kwa wenzetu na kamwe hatutaipata Utulivu wa akili kwa kiingereza wanasema ni peace of mind ndio utuletea amani ya roho na nyinginezo.

Kwa njia ya tahajudi na meditation utapata amani."

Haya ni maneno ya mwaanzao katika MAKALA HII YA KAKA KAMALA ambayo ilieleza kwa kina saana kuhusu TAHAJUDI ama TAAMULI ambayo yeye aliomba tuiite MEDITATION. Kwa namna yoyote ile, alisisitiza kuwa "Ni lazima tuwe na utaratibu wa kukaa mahali patulivu na kujiambia maneno yenye furaha naya kututia amani." Nami June 12,2009 nilizungumzia umuhimu wa kile nilichokiita RIVERSIDE nikirejea wimbo wa Culture (hapa). Bado nikanasa pale kwenye faida ya kujipatia muda binafsi kujiakisi na kuangalia undani wa kile tunachodhani ni matatizo kwetu.
Na leo hii nimerejea kile nilichosikiliza katika kipindi cha Tell Me More cha NPR kinachoongozwa mtangazaji ninayemheshimu na kupenda sana kazi zake redioni Michel Martin na waweza kusikiliza na kusoma mahijiano hayo HAPA
Waweza angalia sehemu ya filamu iliyotengenezwa huko jela ambayo imeanza kuoneshwa jana hapa Marekani kwa kubofya hapa chini


Kilichonigusa na kunifurahisha ni namna ambavyo jela imetumia njia hii isiyo aghali na yenye kugharimu muda wa wafungwa (ambao wangeutumia vinginevyo) kuwafanya waitafute amani ya mioyoni mwao.
Niliwahi kuuliza Kwani kazi ya jela zetu ni ipi???? (Irejee hapa) na japo sijaweza kupata jibu, bado naamini kuwa JELA / VYUO VYA MAFUNZO vyetu nchini Tanzania vinahitaji MAPINDUZI MAKUBWA na kuwa sehemu za kubadili tabia na mienendo badala ya kuwa sehemu za kutesea na kurundika wahalifu na walioingia katika "anga" za "wahalifu safi" (wanaowabambikiza wenzao kesi zisizo za kweli).
Nililojifunza kutokana na kusikiliza kipindi hiki na kuwa tunaweza kubadili maisha ya watu waliotenda yale yasiyokubalika katika jamii kwa kuwafanya wajifikirie mara kadhaa na kuisaka kweli iliyo ndani mwao na iwafanyao wao kuwa wao na kisha kulinganisha walipo na ambapo wangetaka kuwepo ambayo itawafanya watambue pale walipojipoteza katika kutafuta walichodhani wangepata kwa njia iliyowafikisha gerezani.
Na nimesikia namna ambavyo Nguvu hii ya meditation ilivyo na nguvu ya kumfanya mtu kutambua kile ambacho hakuwa akikijua ama kukitambua ama kuwa wazi juu yacho na hivyo kumsaidia kuweza kufanikiwa na pia jamii kufanikiwa kwa mafanikio yake.
Na ndio maana naiona MEDITATION kama NGUVU NDANI MWETU.....YENYE U-SIRI WA MAFANIKIO YETU NA YA WENZETU.
Blessings

JICHO LA NDANI ni kipengele kinachozungumzia mambo mepesi na yaliyo ndani mwetu, ambayo yakiangaliwa vema na kwa tafsiri ama tafakari njema yanaweza ama ndio suluhisho kwa matatizo yetu. Kwa matoleo yaliyopita katika kipengele hiki, BOFYA HAPA

Thursday, February 10, 2011

ELIMU...Labda ni UJINGA BINAFSI unaoendekeza UBINAFSI

Ikiwa utaweza KUSOMA hapa, na pengine kuamua kama utakalosoma ni BUSARA ama UJINGA, basi ujue kuwa nawe umepitia ama kupata ELIMU.
Na kama UMESOMA na kufikia kiwango ch kutotambua kuwa uwazalo wewe ni UJINGA na si lile awazalo umdhaniaye kuwa mjinga, basi ujue kuwa nawe UMELIMIKA.
Kwani....Elimu ni nini? Ni kusoma na kuandika?
Malcom Forbes aliwahi kusem kuwa "Education's purpose is to replace an empty mind with an open one."
SWALI HAPA NI KUWA UNA-REPLACE NA OPEN MIND ILI IJE KUJAZWA NA NANI?
Kwaniiiiiiii....... Umeshawahi kumsoma "MZEE WA UJINGA-BUSARA" (hapa) kisha ukaamua kama kila aandikalo ni UJINGA ama BUSARA ama VYOTE? Haijalishi umewaza nini, kama UMEMSOMA basi utambue kuwa UNA ELIMU (japo elimu ya awali kuweza kusoma) na pia kama ameweza kuandika ujue kuwa naye ANA ELIMU kwani anastahili kuwa na elimu kuweza kuandika.
LAKINI matumizi ya ELIMU ni yapi?
ELIMU ni ile inayomuwezesha mtu kuisaka amani kwa kutumia vita?
ELIMU ni ile inayomuwezesha mtu atengeneze "zana kali" za vita zinazoweza kuua watu wengi kwa mkupuo na kuwatisha wengine?
ELIMU ni ile itakayomuwezesha aliyenayo kujikinga na mizinga na zana kali za minzani wake?
Wcha nikurejeshe kidoogo katika ANDIKO lake Kaka Ndesanjo Macha kuhusu ELIMU YETU, ELIMU KWETU NA ELIMU KWA WENZETU.
Katika makala aliyoyatoa nami kuyanukuu HAPA, akasema "wakoloni walipokuja hawakuchimba kwa undani falsafa na tamaduni zetu. Na wale waliofanya hivyo, walishindwa kutuelewa kwa undani maana, kwanza walikuwa wanatudharau sana, na pili, walikuwa wakiamini kuwa tamaduni zao zilikuwa ni bora zaidi. Wao walikuwa wastaarabu na sisi tulikuwa ni washenzi.
Kwa kuwa waliamini kuwa tamaduni zao ni bora walitumia silaha mbili kuu za kufunga watu minyororo ya utumwa wa akili: elimu na dini. Wakatumia elimu na dini kutusahaulisha yote tuliyokuwa tumerithishwa. Historia yao ikawa ndio yetu. Utamaduni wao ukawa wetu, imani zao zikawa zetu. Watakatifu wao wakawa watakatifu wetu. Kumbukumbu zao zikawa kumbukumbu zetu. Urithi wao ukawa ndio wetu."
Lakini narejea kujiuliza ELIMU NI NINI? ALIYEELIMIKA NI NANI? NA NI KWELI KUWA ELIMU IMFAAYO MTU WA MAGHARIBI NDIYO IMFAAYO WA MASHARIKI?

Labda ni UBINAFSI ambao unamfanya MJINGA kujiona ana ELIMU kwa kupuuza kujifunza (japo) kile aaminicho kuwa ni UJUNGA wa mwenzake.

Labda ni namna nionavyo tatizo, na pengine hilo ndilo tatizo.
Nawaza kwa sauti tuuuu!!!!!!!!!!!!!! (Thinking Out Loud)

Tuesday, February 8, 2011

Familia huishia wapi?


Tumezaliwa watano. Nina dada wakubwa waili na Kaka wadogo wawili. Yamaanisha ni mimi niliye kati. Na sina shaka kuwa wengi tutakubali kuwa hii ni familia. Na kama ambavyo nilishasema, nafurahia saana uhusiano tulio nao baina yetu. Lakini pia kuna Baba na Mama. Nao naamini tutawahesabu kama familia. Nao kila mmoja ana ndugu zake waliozaliwa pamoja. Hao kwao ni familia. Ni kwa mamtiki hiyo nahisi kuwa nao ni familia yetu maana ni familia ya sehemu ya familia yetu. Sasa mjomba na Shangazi wote si wana familia katika miji yao? Na hao ni familia za wazazi wetu na sisi na wazazi ni familia. Ina maana nisiwaite familia?
Najiuliza kama sisi sote si familia kwa mwendo huu na kama sivyo, basi basi naendelea kujiuliza kuwa hivi familia huishia wapi? Ama niseme mtu ni ndugu yako mpaka uzazi upi?

Friday, February 4, 2011

Them, I & Them.....RISE UP....Nasio Fontaine

"Hey! Rise up people Rise up, don’t make them fool you no more......
Wake up people wake up, can’t make them fool you no more.....
Yeah! Power to the people set the captives Free
Freedom is a must, come on and up with the people’s movement
And the people Rise and Say, LIBERATION IS TODAY
And the people Rise and Say POLITICIANS MUST OBEY"
Ni juma jingine ambalo ULIMWENGU umeshuhudia NGUVU YA WANANCHI inavyoendelea kuisumbua dunia. Kama anavyoimba Nasio kwenye wimbo huu kuwa "Power to the people set the captives free", tumeshuhudia namna ambavyo WATU WALIOCHOKA na ambao wanahisi WAMEFIKISHWA MWISHO WA UVUMILIVU wakiamua kulazimisha mabadiliko. Wameamua kuamka na kudai kile kilicho chao. HAKI YAO.
Japo katika kudai haki kuna "wasio haki" wanaotaka kuingia kwa haki za watu ili kuwanyima haki hizo, lakini bado tunaona NGUVU YA UMMA.
Hili si geni. Hili halijaanza kuonekana na kusemwa leo. Kwenye ukurasa ama "label" hii ya I & THEM tumeandika kuhusu UKWELI ULIOPO KWENYE ROOTS REGGAE katika kueleza matatizo ya watu. Ukweli ambao unaendelea kubaki na kweli yake miaka mingi baadae kwa kuwa MATATIZO BADO YAPO. Ukifuatilia kipengele hiki utatambua nisemalo.
Lakini leo turejee yanayotokea Misri, Tunisia, Yemen, Jordan na kwingine ambako watu wameamua (ama pengine kuamulishwa ama kusaidiwa kuamua) kuondoa UTAWALA uliopo na kuleta mwingine kwa tumaini la kuwa \utakuwa na manufaa kwao.
Basi Ijumaa hii nisiwe na maneno mengi, natambua kama (hata kwa bahati mbaya) umefuatilia habari, utajua ninalozungumzia. Je! Wanasiasa wata"OBEY" kulingana na haya yanayotokea?
Msikilize Nasio Fontaine na kibao chake RISE UP kutoka albamu ya LIVING IN THE POSITIVE ya mwaka 2003.

Kwa wale msomeao kwenye mitandao isiyoonyesha "player", BOFYA HAPA kuusikiliza kutoka nilipouhifadhi.
Yeah! Rise up ye Mighty people
We gonna Rise up uhh
We gonna Wise up, yeah!
We gonna Wake up
Come on! You Mighty people

Hey, Rise up people Rise up, don’t make them fool you no more
Nuh, no, no, no, no, no, no, no, no
Wake up people, Wake up come on!
Can’t make them fool you more more. Nuh,
Liberation is a must
Yeah! Power to the people set the captives Free
Freedom is a must.
Come on and up with the people’s movement
And the people Rise and Say, liberation is today.
And the people Rise and Say, FREEDOM IS TODAY

We gonna Rise up come on!
We gonna Wise up, uuhh!
We gonna Wake up
Rise up Mighty people
We gonna Shake up
Pah dap, pah, pah, pah, pah, dap, pah

Hey! Rise up people Rise up, don’t make them fool you no more
No, no, no, no, no, no, no, no, no, no, no
Wise up people wise up, can’t make them fool you no more
People are rising up fighting for freedom
Force of the people is on the rise.

Hey, Rise up people Rise up, don’t make them fool you no more
Nuh, no, no, no, no, no, no, no, no
Wake up people, Wake up!
Can’t make them fool you more more. Nuh,
Yea! Break the Chains things must be rearranged
Up you Mighty race accomplish what you will
And the people Rise and Say LIBERATION IS TODAY
And the people Rise and Say Politicians must obey

We gonna Rise up, come on ye mighty people
We gonna Wise up, liberation is a must
We gonna wake up huhh, come on, come on
We gonna Shake up,
Cause you’ve been kept down for so long, yeah,
And the people Rebel, we’re gonna Win now
And the people Rebel. Revolution time
And the people Rebel, Lord, Lord, Lord
Yes the people Rebel, yes and the people rebel
Yeah! And the people rebel, Ras Tafari Live


**Them, I & Them ni kipengele kikujiacho kila Ijumaa kinachoelezea kazi za wasanii (Them) kulingana na maono yangu (I) kwa ajili na manufaa ya hadhira (Them)**
Kwa nyimbo zaidi ndani ya kipengele hiki bofya hapa.
IJUMAA NJEMA

Thursday, February 3, 2011

Labda hatuendelei kwa kuwa "wa kutuendelesha" hayupo kwenye "kiendelesheo" chetu (Prt 3)

Photo Credits:Jimmy Falon Blog
Natambuwa kuwa TUNA TAFSIRI TOFAUTI ya neno ama kitu MAENDELEO. Lakini haijalishi unatafsiri vipi, tutakubaliana kuwa SI KILA MABADILIKO NI MAENDELEO JAPO KILA MAENDELEO NI MABADILIKO.
Na kwa sehemu yoyote iliyo na maendeleo, utagundua kuwa ni wachache wafanyao maamuzi yanayoleta maendeleo hayo na ambao wakati mwingine wakati wafanyapo haya, hupuuzwa (kwa kuwa wengi wetu husita kubadilika). Kwa maana nyingine ni kuwa kwa maendeleo yoyote kufanyika, ni lazima wale wachache (ambao mara nyingi wamepewa ama kujipa dhamana) wanatakiwa kuwa makini katika kufanya maamuzi yao kwa manufaa ya nchi na wananchi.
Hawa (wafanya maamuzi) wanapokuwa na mtazamo mwingine, wanapokuwa wanawaza vingine, wanapojiweka katika ngazi ama hatua nyingine na wale wanaostahili kuwa nao, hawawezi kufanya maamuzi yawafaao kwa kuwa HAWANA MAHITAJI YAFANANANYO NAO. Kwa hiyo maendeleo kwao ni tofauti na maendeleo kwa wawaongozao.
Na ni hapo tunapokuja kuona mifano kadhaa.
1: Maendeleo yetu ni pamoja na KUTHAMINIWA.
Lakini tunaona namna ambavyo thamani ya mTanzania inavyokuwa kulingana na uajiri alionao, ama mahusiano kati yake na wakubwa mahala fulani. Hivi majuzi tumesikia habari ya WATOTO KUMI WALIOUKULIWA KWENYE SHIMO LA TAKATAKA huko Mwananyamala. Hiki kitendo kilitakiwa kupingwa na kufanyiwa uchunguzi wa hali ya juu. Hawa watoto hawakutendewa haki (hata kama walizaliwa wakiwa wafu) kwani kama viumbe na kama waTanzania, bado walikuwa na haki ya kupata HESHIMA ZOTE ZA MWISHO na kuzikwa kulingana na mila, desturi na imani za asili waliyorithi. Lakini hakuna aliyesikika akionekana kuwekeza ktika KUWAJIBISHA WATAKAOBAINIKA KUTENDA KITENDO HIKI CHA FEDHEHA.
Hawa walikuwa na bado ni waTanzania. Hazikuwa TAKWIMU. Hivi majuzi walipouawa watu Arizona tuliona Rais wa Marekani akienda kufariji.. Labda Rais wetu alikuwa "busy", lakini ni lini wanaotenda makosa kama haya wamewajibishwa?
Labda "waendeleshaji" wetu hawako kwenye "kiendelesheo" cha UTU NA THAMANI YA MTANZANIA kwani wangekuwa huko, wangemtafuta mhusika na kumuadhibu. HAWA WATOTO HAWAKUJIZIKA.
2: ADHA YA MIUNDOMBINU
Hakuna ubishi kwamba viongozi (ama niseme WATAWALA) hawatumii aina ya miundombinu tunayotumia sisi. Niliwahi kuandika kuhusu BARABARA ZETU (irejee hapa) , na mara kadhaa nimezungumzia suala la AJALI (rejea hapa). Haya yote licha ya kuwa yanachangia kuondoa nguvukazi ya jamii na kuzorotesha maendeleo ya nchi, WAHUSIKA HAWAJALI kwa kuwa wao si watu walio katika mfumo wetu wa maisha. Wakati sisi "tunalia" na foleni katikati ya jiji, wao wanafikiria kuanzisha huduma za helikopta za kukodi (as if zitamfaa aliye Mbagala ama Gongo la mboto ambaye ndiye mwenye uhitaji mkubwa wa kuondokana na foleni). Hawasafiri kwa barabara tupitazo sisi kwenda vijijini na ndio maana HAWAONI UCHUNGU NA ADHA YA UBOVU WAKE.
Siamini kama WANAPATA MGAO tunaosikia kila siku kwa ndugu zetu, na ndio maana hawana "LADHA HALISI" ya tatizo la kukatika kwa umeme. Hawatumii "line" za maji tutumiazo sisi, na ndio maana mabomba yao yakitoa maji masaa 24, hawajui kuwa kuna yanayomaliza miezi (kama sio miaka) bila kupitisha unyevu ndani mwake.
NI KWA KUWA HAWAKO KWENYE MIUNDOMBINU YETU, HAWAJUI ADHA ZETU.
3: ADHA YA HUDUMA ZA JAMII
Labda wangekuwa wanatibiwa atibiwako bibi yangu, ama kupata chakula apatapo mpwa wangu. Lada wangekuwa wanatambua adha hizi. Labda watoto wao wangesoma tuliposoma sisi wangethamini mazingira ya shule zetu, na labda wangekuwa wakikaa mahabusu wakaazo "wasingiziwa" wengine wangejua haki ya mtuhumiwa (kuwasi mkosaji mpaka atakapokutwa na hatia na mahakama)
Lakini kwa kuwa wao hupata dhamana hata kama kosa lao ni kubwa, kwa kuwa wao ksi zao huenda mwendo kasi, kwa kuwa wao hutibiwa nje, hufunga barabara waendapo vijijini, husafiri kwa ndege, husomesha nje ya chi, HAWAJUI MAHITAJI YETU KWA KUWA HAWAKO KATIKA NGAZI MOJA NASI.
Na haya ni machache ambayo yananifanya niingie katika sehemu hii ya tatu nikiwaza kuwa Labda hatuendelei kwa kuwa "wa kutuendelesha" hayupo kwenye "kiendelesheo" chetu
NAWAZA KWA SAUTI TU!!!!!!

Tuesday, February 1, 2011

Hotuba ya Mhe. Balozi Maajar..VIDEO

Wasipokuwa wao bila wewe, labda nawe si wewe bila wao.

MAISHA NI UTEGEMEZI. Ndio maana licha ya kuwa kuna wanaojiona kama "vichwa vya familia", bado wao si wao peke yao, bila hao wawaonao "mikia". Kwa maana nyingine, familia haiwi familia ikiwa na mtu mmoja. Ni lazima uwe na mwenzako / wenzako ambao uwepo wao na utayari wa kukuacha umiliki "u-kichwa" ndio ukufanyao uwe na "hadhi" uliyonayo.
Labda tuhame toka kwenye familia tuingine kwenye sanaa.
Kwenye fani hiyo (na hasa nchini mwangu Tanzania), ninawaona na kuwagawa wasanii katika makundi mawili. Wasanii HALISI wanaofanya kazi wakizingatia MISINGI YA KAZI na kisha kuna wale wanaojibidiisha kupata SIFA ambazo huwawezesha "kutumiwa" na kisha kujipatia sehemu ya mapato halali waliyostahili.
Wale wawekezao kwenye bidii na misingi ya kazi ni wengi japo hawafahamiki miongoni mwa wasiojua snaa halisi (ambao nao kwa bahati mbaya ni wengi zaidi na wamechukua majukumu ya kutambua, kutambilisha na kutunuku sanaa). Wasanii hao nawambia HERI KWAO kwani hawatachuja.
Kwa ndugu ambao sanaa kwao huambatana na SIFA, MATAMASHA, USHABIKI WA MITAANI nk, wanasahau kuwa licha ya kuwa wao ndio watajwao, bado ni kwa MSAADA wa wengine wanaoshiriki katika ufanikishaji wa sifa zao. Labda kwa ndugu wanaofahamu utayarishaji na urushaji wa vipindi vya Televisheni watatambua kuwa Anderson Cooper asingekuwa maarufu alivyo kama si mlolongo wa wafanyakazi wengi wanaofanya kazi kutwa-kuchwa "nyuma ya pazia" kufanikisha afanyalo. Na mara zote utasikia juhudi za kuwathamini na kuwaweka waandishi, wazalishaji, wapiga picha, waongoza kamera nk japo sisi hatuwaoni na kuwajua. Na hao ndio hasa wafanyakazi na yule asimamaye mbele ya kamera ni "kipaji" (talent) tu.
Kwa wanamuziki / wasanii wa nyumbani ni lazima watambue kuwa uongozi wa bendi, wana-bendi wengine nk ndio wawafanyao wao watambulike, waheshimike na hata "wapendwe" na kusemwa walivyo sasa. Lakini wengi wao husahau hilo na kuanza KUPIMA MASLAHI KWA KUTUMIA KELELE ZA MASHABIKI. Yaani kwao, wingi wa mashabiki (ambao kwa bahati mbaya hufuata upepo) ndio kiburi chao cha maslahi. Hutumia hilo kudai maslahi zaidi na / ama kutafuta maslahi zaidi kwingine. Tatizo ni KINACHOFUATA baada ya kuondoka toka kwa wale wanaokufanya uwe mashuhuri kwa namna ulivyo.
NISEME WAZI KUWA MARA NYINGI WASANII HAWA HUWA NA KIPAJI AMA UWEZO WA HALI YA JUU KATIKA JAMBO MOJA AMA MAWILI KATI YA MENGI YANAYOHITAJIKA ILI KUFANIKIWA KATIKA MUZIKI
Photo Credits: Bongocelebrity.com
-Labda ni "watunzi" wa nyimbo nyingi / zote katika albamu
-Labda ni "wapanga alaP wazuri katika nyimbo za bendi zao.
-Labda wana "sauti nzuri" zaidi ya wengine.
-Labda watoa ni "watoa maoni" yanayonogesha nyimbo nyingi n.k
Lakini la kutambua ni kuwa MAFANIKIO KATIKA MUZIKI NI ZAIDI YA HAYO na hata mengine mengi. Na ni mpaka wasanii watakapotambua kuwa kutunga, kupanga ala, sauti nzuri, nk. sio vitu pekee vinavyohitajika katika kufanikiwa ki-muziki, basi wataendelea "kupanda na kushuka" katika kile wakisakacho kwani kwa kutotambua watafutalo, wanajikuta wakijipoteza kwenye harakati za kujitafuta.
Na mifano halisi ni kama hii ifuatayo. Hebu sikiliza wimbo kama MASIMANGO wa TOT Plus ambao uliimbwa na kina Banzastone, Waziri Sonyo, Mhina Panduka, Abdul Misambano nk, na sasa jiulize hawa wasanii wako wapi sasa?

Pia hawa walishiriki katika wimbo mwingine hapa chini wa ELIMU YA MJINGA na zisikilize uone UMOJA wao ulivyokuwa muhimu kuwafanikisha na namna ambavyo UTENGANO wao UMEWAPOTEZA.

Ama labda sikiliza wimbo MTUMAI CHA NDUGU

na hata MAISHA KITENDAWILI

ambamo Mwinjuma Muumini, Badi Bakule, Amina Ngaluma na wengine wameshiriki. Hawa wote wameonesha ujuzi wa hali ya juu katika kuimba nyimbo hizi (kama timu), lakini tazama walipo kwa sasa.
LABDA WASANII WANGEJIFUNZA TOKA KWA KUNDI HILI LA KILIMANJARO BAND ama Wana Njenje
Ambalo takribani kila mmoja ana uwezo wa kufanya kazi kivyake na asilale njaa, lakini umoja wao umewafanya wawe na mafanikio na kujijengea heshima miongoni mwa washabiki duniani kote.
NAWAZA KWA SAUTI TUUUU!!!!